Alhamisi, 1 Septemba 2016
RAIS JOHN MAGUFULI KUBADILISHA FEDHA
Katika kilekinachoonekana kutaka kuwadhibiti watu wanao daiwa kuficha fedha, Rais John Magufuli amesema kwa mamlaka aliyonayo anaweza kuamua kubadilisha fedha ili zile znazofichwa na watu hao wakose mahali pakuzipeleka.
Akizungumza katika mkutano wa 14 wa mwaka wa waandisi ulio fanyika katika ukumbi wa mlimani city leo mchana mjini DAR ES SALAM, Magufuli amesisitiza kuwa kauli hiyo nimahususi kwa watu walio ficha fedha katika majumba yao na kuwataka kuwachana na tabia hiyo mara moja ili fedha hizo ziingie katika mzunguko.
Huku akisisitiza kuwa katika utawala wake fedha za bure hazitakuwepo kwa sababu zilizokuwepo awali zilitokana na fedha za wizi kutoka serekalini ambazo kwa sasa zimezibitiwa, alisem kwa mwendo anaokwenda nao sasa ni ngum kwa mwananchi kupata fedha bila kufanya kazi.
About Unknown
Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.
